Monday, January 10, 2011

JINSI YA KUPUNGUZA MAFUTA MWILINI

Habarini ya leo nduguzanguni

leo hii napenda kuwaeleza dawa au juice mpya kwa ajili ya kupunguza mafuta mwilini.
hii juice si kama inapunguza mafuta mwilini tu bali pia kama umekosa kwenda haja
kubwa badala ya kutumia mapapai pia unaweza kutumia juice hii

vitu vinavyohitajika katika kutengeneza juice hii
1. ukwaju kilo moja
2. maji safi na salama lita 3.
3. Asali kiasi tu (hii inatumika badala ya sukari).

JINSI YA KUTENGENEZA.

Chukua ukwaju na weka katika chombo kisafi kikubwa cha kuweza kutosha kutengenezea hiyo juice yako.
weka maji lita 2
acha uloane kwa mda wa masaa manne hadi matano
nawa mikono yako
fikicha ule ukwaju na utoe mapeke.
chukua lita moja ya maji uliyobakiza na uweke tena kwenye juice yako ili ikamilike lita 3.
chuja juice yako
ukiwa umeshachuja kwa umakini chukua asali na uweke kisha koroga kwa mda mrefu kama dk 5 hadi 10
ili juice yako ichanganyike vizuri na asali.
kipimo cha asali utaangalia mwenyewe kama inatosha au la kwani ni badala ya sukari kwa hiyo unaweza kukadiria.
ikishakuwa tayari unaweza weka kwenye kidumu au kwenye chombo unachoona wewe kinafaa kisha weka kwenye fridge ipoe kidogo.
tumia grass moja asubuhi na grass moja jioni kabla ya kulala.

TAHADHARI:. baada ya kunywa hii juice utaharisha sana tena sana ila tumbo halitakuuma na huwezi pata mazara yeyote zaidi ya kuharisha. kwa hiyo ukijua umetumia hii juice jaribu kukaa karibu na toilet mda wote na tishu ziwepo kwa wingi. maana ni full maharibiko katika tumbo lakini ni dawa nzuri sana sana.

7 comments: