Friday, June 24, 2011

BINTI MWENYE ULIMI MREFU DUNIANI


Binti Annika Irmler (pichani juu) ambaye ni raia wa Ujerumani ana umri wa miaka 16 ndiye mwanamke mwenye ulimi mrefu zaidi duniani kwa mujibu wa Kitabu cha Rekodi za Dunia za Guinness.

Binti huyo ambaye alivunja rekodi hiyo mwaka 2007 ni mwanafunzi wa sekondari, wakati huo alipokuwa anavunja rekodi alikuwa umri wa miaka 12.

Kwa ufahamu zaidi, mrembo Annika ana ulimu wenye urefu wa sentimita 7.6.  Utakuwa huna ubishi kama utatazama picha inayoonyesha kipimo hicho.

Annika anasema: “Sijui sana kuhusu ndimi, huenda ulimi wangu ukaendelea kurefuka.  Hata hivyo, nafurahi walimwengu wengi wananifahamu sasa kupitia ulimi huu.”

Kwa kina kaka na kina dada wanaopenda kurefusha ndimi zao, nafikiri teknolojia ya sasa inawezesha hivyo, kwani kuna utaalam mwingi tu wa kukuza viungo vingi vya mwili.
Kujaribu si vibaya, kwani kutojaribu ni kushindwa tayari. hahahahahahahahaaaaaaaaaaaaa!..... yangu macho ngoja nitafute na mwanaume aliyevunja rekodi.

No comments:

Post a Comment